DJ RODGER
ABM RADIO
Saturday, February 1, 2014
FAHAMU:SAKI STARS BAND KUTOKA DODOMA BEND INAYOKUJA KULETA MAPINDUZI KWENYE DANSI TANZANIAA
Uongozi
wa Bendi muziki wa dansi ya Saki Stars bendi aka Vijana Wa kazi kutoka mkoani Dodoma,
umesema kuwa umeamua kufanya muziki kwa kuzingatia ubunifu, tofauti na
zilivyo bendi nyingine za muziki huo ili kukamata soko muziki hapa nchini.
Bendi hiyo makazi yake mjini Dodoma inaundwa na wanamuziki
kama vile-- Jay Z,Prezdaa Venance, Kibon Mangwela na wengine wengi
LA LIGA: BARCA YAPIGWA NOU CAMP!
LA LIGA sasa ni mshikemshike kweli baada
ya Leo Valencia kufanya kweli Uwanjani Nou Camp na kuichapa Barcelona
Bao 3-2 na kuwaweka Mabingwa hao kwenye njia panda maana Jumapili
Atletico Madrid au Real Madrid zina nafasi kubwa kuwapiku uongozi wa
Ligi.
+++++++++++++++++++++++++++++++
MSIMAMO-Timu za Juu:
| NA | TIMU | P | W | D | L | F | A | GD | PTS |
| 1 | FC Barcelona | 22 | 17 | 3 | 2 | 59 | 16 | 43 | 54 |
| 2 | Atletico de Madrid | 21 | 17 | 3 | 1 | 52 | 14 | 38 | 54 |
| 3 | Real Madrid CF | 21 | 17 | 2 | 2 | 60 | 21 | 39 | 53 |
| 4 | Athletic de Bilbao | 21 | 13 | 3 | 5 | 41 | 27 | 14 | 42 |
+++++++++++++++++++++++++++++++
POLISI WATANO WAFARIKI PAPO HAPO BAADA AJALI YA GARI DODOMA
Baadhi ya wananchi wakiangalia gari hilo, lililopata ajali na kuua askari hao.
Gari hilo lililopata ajali na kuua askari hao.
Na. Sylvester Onesmo wa Jeshi la Polisi Dodoma.
Askari
polisi watano mkoani dodoma wafariki dunia papohapo katika ajali ya
gari iliyotokea 31/01/2014 majira ya 23.45 hrs katika barabara kuu ya
Dodoma – Morogoro eneo la Mtumba Center, Kata ya Mtumba Tarafa ya
Kikombo Manispaa ya Dodoma, ambapo gari namba T.770 ABT Toyota Corolla
lililokuwa likiendeshwa na Askari namba H. 3783 PC DEOGRATIUS wa Polisi
Wilaya ya Kongwa likitokea Dodoma mjini likielekea Wilayani Kongwa
liligongana uso kwa uso na gari namba T.997AVW Scania Bus mali ya
Kampuni ya Mohamed Trans lililokuwa likiendeshwa na JUMA s/o MOHAMED,
miaka 38, Mkazi wa Mwanza, likitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma na
kusababisha vifo kwa askari watano papohapo.
Subscribe to:
Posts (Atom)




